Huyu ndio Elizabeth ‘Lulu’ Michael, na haya ndio aina ya malezi tuliyokuwa tukimpati
Kupitia kwenye vibaraza mbalimbali vya wadau wa Jukwaa Huru sanjari na wadau wangu katika kurasa zangu mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii, hapa ni sehemu ya mkusanyiko wa picha zenye kumuonyesha binti Elizabeth Michael, maarufu kama Lulu, na aina ya maisha ambayo tulikuwa tukimkuza kama taifa, kama wanahabari, kama wanajamii na kama Mtanzania mmoja mmoja.




Naam, huyu ndio binti yetu Elizabeth Michael, maarufu kwa jina la Lulu, ambaye hivi sasa sisi ambao tumempa makuzi ya namna hiyo hapo juu, ndio sisi ambao tunatamani mbingu zingetoboka na atumbukie kwenye tanuri la moto wa jehanam kisa “kanuua” Kanumba. Baada ya mazingira ya namna hiyo, kweli tunamtendea haki kumuombea mabaya? Na hiyo ni sehemu ndogo mno ya malezi tuliyokuwa tukimpatia.
Ninawaza kwa maandishi tu, na mawazo yangu yanaweza kuwa sawa na ya mwingine mwenye kuwaza sawa na mimi au tofauti na mtu anayewaza kinyume na mimi.
Huyu ndio Elizabeth 'Lulu' Michael, na haya ndio aina ya malezi tuliyokuwa tukimpatia ,
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni
Zingatia: Mwanachama wa blogu hii tu ndiye anayeweza kuchapisha maoni.